YANGA YAENDA ZANZIBAR KUISUBIRI FAR RABAT MECHI JUMAMOSI AMAN

YANGA YAENDA ZANZIBAR KUISUBIRI FAR RABAT MECHI JUMAMOSI AMAN

 

KIKOSI cha Yanga SC kimeondoka mapema leo kwenda Zanzibar kwa matayarisho ya ‘mwisho mwisho’ ya mchezo wake wa kwanza wa Kund B Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco Jumamosi ya Novemba 22 Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
Ikumbukwe Jumamosi Yanga ilichapwa mabao 3-2 na KMC FC katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Gymkhana, Dar es Salaam – mabao ya KMC yakifungwa na Daruwesh Saliboko mawili na beki Nickson Joseph Mosha moja, wakati ya Yanga yalifungwa na viungo na Mkongo Maxi Mpia Nzengeli na Mguinea, Balla Moussa Conte.

Post a Comment

0 Comments